AM ZE GCR

Tuesday, May 14, 2013

EDWIN SHILLA:NYIMBO MOJA STUDIO MBILI

Rapper wa injili kutoka mji kasoro bahari Moro town Edwin Shillah ameifungukia
blog hii kwamba yuko mbion kuachia  ngoma yake mpya ambayo kiukweli bado anaitafutia jina japo kuna uwezekano wa kuipa jina la Safisha,ambao amezungumzia zaidi kuhusu kujihoji mbele za MUNGU,ambao ametumia kujihoji yeye mwenyewe kuwawakilisha wengine akitolea mfano wa tabia ya waimbaji kupenda  kuhudumu kanisan na kuondoka bila hata kutaka kusikiliza neno.
 Shillah ambae ametupia ngoma kadhaa mtandaoni kwenye www.reverbnation.com/shillah
amesema ngoma hiyo imefanyika na studio mbili tofauti ambayo moja ni ya Moro na nyingine ni studio ya Dar,"Wimbo huo unafanyika katika studio mbili tofauti ambapo Moja iko Dar-es-Salaam chini ya producer Dupah na ya pili ipo Morogoro inaitwa Uptown Music chini ya producer King Niver.

Nawasihi watu kukaa mkao wa kupokea ujumbe kwa kujifunza na kuburudika na kubarikiwa kwani iko na vionjo vya tofauti sana ambapo kuna R&B katika Chorus ambayo imesimamiwa na kuimbwa vilivyo na Chorus Killer wangu ambaye ni Lenny B. Pia verse nimeziimba mwenyewe kwa maadhi ya Hip Hop Commercial kali na sauti iloshiba.

Naamini ni moja ya nyimbo ambayo italeta changamoto sana katika tasinia ya music wa injili wenye maadhi ya hip hop Tanzania na africa ya Mashariki.
Napatikana kwa contact No. +255712 247560 / +255762 247560",alifunguka
Shilla kupitia facebook account yake ambayo ni www.facebook.com/edwinshillah.