AM ZE GCR

Wednesday, May 15, 2013

JICHO LA TATU.....KIPIMO HALISI CHA MAFANIKIO YAKO,BY FARAJA MNDEME

                                 

                                                                SUCCESS & FAILURE.

1.Kuna kamtazamo fulani ambako watu wengi tunako kuhusu Mafaniko kwenye maisha yetu ambako Muda mwingine kanatupoteza na kutufanya tukose mwelekoo kwenye maisha yetu ya kila siku.

"Mafanikio kwenye maisha sio yale ya kujilinganisha na mtu mwingine,Mafanikio ni hali ya kuweza kufikia lengo fulani kwenye maisha au jambo lolote ambalo umejiwekea.Mfano Ulipanga Upate Million 100 kwa Mwaka na Ukafanikiwa Kupata Million 70 wewe umeshindwa haukufanikiwa kwenye lengo Lako.Angalizo Unaweza ukawa umewapita watanzania wengi kupata milioni 70 kwa Mwaka lakini Ukilinganisha na Malengo yako ya Kupata Million 100 kwa Mwaka wewe bado umeshindwa kufikia lengo.
Kipimo cha Mafanikio kwenye Miasha sio Mtu Mwingine umemzidi Mara ngapi.Kipimo Halisi cha Mafinikio ni wewe mwenyewe je Umefikia malengo yako kiasi gani.Wewe ndio Kipimo cha mafikio yako Binafsi ingawa wengine wanaweza kukuona Umefanikiwa

2.Kushindwa ni hali ya kutoweza kufikia malengo fulani kwenye maisha wewe binafsi na sio kujilinganisha na mwingine.Unaweza Ukawa unafanya vizuri kwenye jambo fulani lakini ukilinganisha na uwezo ulio nao kulingana na wengine kumbe ungefanya vizuri zaidi.Kushindwa kwenye jambo haitegemei umewapita watu mara ngapi kwenye hiko kitu/jambo bali wewe umetimiza lengo lako wewe binafsi kwenye malengo yako.Machoni Petu unaweza kuwa umefanikiwa lakini Ukieenda kwenye ile idadi ya Malengo yako kumbe haujafanikiwa..Pia machoni mwetu tunaweza kuona umeshindwa kumbe wewe ndio umefanikiwa kufikia malengo yako kulingana na kpimo chako wewe Binafsi.Kushindwa kufikia malengo fulani hakutegemei kujilinganisha na wengine.Wewe ndio kipimo cha Kushindwa kwako juu ya jambo fulani.

....Kipimo Halisi cha Mafanikio au Kushindwa ni Kile cha Kwako Binafsi Ulichojiwekea kulingana na Uwezo uliokuwa nao na sio Kile ambacho Unatumia kujilinganisha na wengine....

Tumeshaimaliza Robo ya kwanza ya Mwaka na ya Pili ndio Ipo Ukingoni ..jiulizee...

#Above The Limits#